Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Wasiwasi waibuka huku M23 ikiunda utawala mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

 


Kundi la waasi la M23 limeteua utawala wake katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wake mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na hivyo kuzua wasiwasi

Katika taarifa ya kundi hilo, kiongozi wa kisiasa wa M23 Bertrand Bisimwa amesema kundi hilo limeteua watawala katika eneo la Rutshuru la Kivu Kaskazini.

Aliongeza kuwa viongozi wa miji ya Kiwanja, Rubare na Bunagana, katika Kivu Kaskazini, wameteuliwa pia.

Waasi wanadhibiti sehemu kubwa ya Rutshuru na Masisi, mbili kati ya wilaya tano zinazounda jimbo la Kivu Kaskazini, na ziko takriban kilomita 35 (maili 22) magharibi mwa mji mkuu wa mkoa huo, Goma.

Katika siku za hivi karibuni, jeshi la Congo limeanzisha mashambulizi makubwa ya ndege zisizo na rubani katika maeneo yanayodhibitiwa na M23.

Siku ya Jumatano msemaji wa kundi hilo alisema wapiganaji wake waliiangusha moja ya ndege zisizo na rubani tatu zilizokuwa zikitumiwa na jeshi.

BBC haijathibitisha dai hili kwa duru huru, wala jeshi halijatoa maoni kulihusu.

Mitandao ya kijamii ya Kongo imekuwa ikijibu kuhusu M23 kuteua utawala wake katika Kivu Kaskazini.

Baadhi wanaona huo ni mwanzo wa hatua ya kuunda jimbo tofauti mashariki mwa Kongo, huku wafuasi wa M23 wakisema ni haki ya kundi hilo kutawala maeneo yanayodhibiti.

SOMA ZADI


Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

INSIGNIA LIMITED COMPANY

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)