Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Wasiwasi waibuka huku M23 ikiunda utawala mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

 


Kundi la waasi la M23 limeteua utawala wake katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wake mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na hivyo kuzua wasiwasi

Katika taarifa ya kundi hilo, kiongozi wa kisiasa wa M23 Bertrand Bisimwa amesema kundi hilo limeteua watawala katika eneo la Rutshuru la Kivu Kaskazini.

Aliongeza kuwa viongozi wa miji ya Kiwanja, Rubare na Bunagana, katika Kivu Kaskazini, wameteuliwa pia.

Waasi wanadhibiti sehemu kubwa ya Rutshuru na Masisi, mbili kati ya wilaya tano zinazounda jimbo la Kivu Kaskazini, na ziko takriban kilomita 35 (maili 22) magharibi mwa mji mkuu wa mkoa huo, Goma.

Katika siku za hivi karibuni, jeshi la Congo limeanzisha mashambulizi makubwa ya ndege zisizo na rubani katika maeneo yanayodhibitiwa na M23.

Siku ya Jumatano msemaji wa kundi hilo alisema wapiganaji wake waliiangusha moja ya ndege zisizo na rubani tatu zilizokuwa zikitumiwa na jeshi.

BBC haijathibitisha dai hili kwa duru huru, wala jeshi halijatoa maoni kulihusu.

Mitandao ya kijamii ya Kongo imekuwa ikijibu kuhusu M23 kuteua utawala wake katika Kivu Kaskazini.

Baadhi wanaona huo ni mwanzo wa hatua ya kuunda jimbo tofauti mashariki mwa Kongo, huku wafuasi wa M23 wakisema ni haki ya kundi hilo kutawala maeneo yanayodhibiti.

SOMA ZADI


Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)