Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Mnada wa vitu vya Mandela: Afrika Kusini yataka kuzuia uuzaji juu ya urithi

 


Serikali ya Afrika Kusini inajaribu kusitisha mnada wenye utata wa vitu 70 vya kibinafsi vya shujaa wa kupinga ubaguzi wa rangi Nelson Mandela.

Ni pamoja na seti ya vifaa vya usikivu, kitambulisho, zawadi kutoka kwa viongozi wa dunia na baadhi ya mavazi ya rais wa kwanza wa kidemokrasia, kama vile mashati yake ya "Madiba".

Binti yake mkubwa, Makaziwe Mandela, anapiga mnada bidhaa hizo nchini Marekani.

Lakini serikali ya Afrika Kusini inasema bidhaa hizo ni mali ya taifa hilo.

Chini ya sheria ya nchi, vitu vinavyochukuliwa kuwa vya urithi wa kitaifa haviwezi kuchukuliwa nje ya Afrika Kusini.

Wakala wa Rasilimali za Urithi wa Afrika Kusini (Sahra), chombo cha serikali kilichopewa dhamana ya kulinda historia na utamaduni wa nchi hiyo, kilisema kuwa kimewasilisha rufaa ya kuzuia uuzaji huo.

Ombi hilo limeungwa mkono na wizara ya michezo, sanaa na utamaduni. Waziri Zizi Kodwa alisema anaunga mkono kesi hiyo "kwa ajili ya kudumisha urithi tajiri wa nchi".

Aliongeza kuwa kuzuia uuzaji huo ni muhimu kwani Mandela "ni muhimu kwa urithi wa Afrika Kusini".

"Kwa hivyo ni muhimu kwamba tuhifadhi urithi wa Rais wa zamani Mandela na kuhakikisha kwamba uzoefu wa maisha yake wa kazi unabaki nchini kwa vizazi vijavyo."

Serikali ilipinga mnada huo ulipotangazwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2021, ikisema kwamba baadhi ya bidhaa zilizopendekezwa kuuzwa ni za sanaa za kitaifa.

Kama matokeo, mnada wa awali, ambao ulikuwa umepangwa kwa 2022, ulighairiwa na vita vya kisheria vya miaka miwili vikafuata.

Mwezi uliopita, Mahakama Kuu ya Pretoria hatimaye ilimpa Bi Mandela idhini ya kuuza bidhaa hizo, ikipinga hoja ya serikali kwamba ni za urithi wa kitaifa.

SOMA ZAIDI


Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)