Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Mnada wa vitu vya Mandela: Afrika Kusini yataka kuzuia uuzaji juu ya urithi

 


Serikali ya Afrika Kusini inajaribu kusitisha mnada wenye utata wa vitu 70 vya kibinafsi vya shujaa wa kupinga ubaguzi wa rangi Nelson Mandela.

Ni pamoja na seti ya vifaa vya usikivu, kitambulisho, zawadi kutoka kwa viongozi wa dunia na baadhi ya mavazi ya rais wa kwanza wa kidemokrasia, kama vile mashati yake ya "Madiba".

Binti yake mkubwa, Makaziwe Mandela, anapiga mnada bidhaa hizo nchini Marekani.

Lakini serikali ya Afrika Kusini inasema bidhaa hizo ni mali ya taifa hilo.

Chini ya sheria ya nchi, vitu vinavyochukuliwa kuwa vya urithi wa kitaifa haviwezi kuchukuliwa nje ya Afrika Kusini.

Wakala wa Rasilimali za Urithi wa Afrika Kusini (Sahra), chombo cha serikali kilichopewa dhamana ya kulinda historia na utamaduni wa nchi hiyo, kilisema kuwa kimewasilisha rufaa ya kuzuia uuzaji huo.

Ombi hilo limeungwa mkono na wizara ya michezo, sanaa na utamaduni. Waziri Zizi Kodwa alisema anaunga mkono kesi hiyo "kwa ajili ya kudumisha urithi tajiri wa nchi".

Aliongeza kuwa kuzuia uuzaji huo ni muhimu kwani Mandela "ni muhimu kwa urithi wa Afrika Kusini".

"Kwa hivyo ni muhimu kwamba tuhifadhi urithi wa Rais wa zamani Mandela na kuhakikisha kwamba uzoefu wa maisha yake wa kazi unabaki nchini kwa vizazi vijavyo."

Serikali ilipinga mnada huo ulipotangazwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2021, ikisema kwamba baadhi ya bidhaa zilizopendekezwa kuuzwa ni za sanaa za kitaifa.

Kama matokeo, mnada wa awali, ambao ulikuwa umepangwa kwa 2022, ulighairiwa na vita vya kisheria vya miaka miwili vikafuata.

Mwezi uliopita, Mahakama Kuu ya Pretoria hatimaye ilimpa Bi Mandela idhini ya kuuza bidhaa hizo, ikipinga hoja ya serikali kwamba ni za urithi wa kitaifa.

SOMA ZAIDI


Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)