Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Jaribio la Marekani kurejea mwezini katika miaka 50 lagonga mwamba

 




Chombo cha anga za juu cha Marekani kilichozinduliwa wiki iliyopita kujaribu kutua Mwezini kimesitisha ujumbe wake baada ya kulipuka juu ya Bahari ya Pasifiki.

Chombo hicho kwa jina Peregrine One kilipata hitilafu ambayo iliharibu matarajio yoyote ya kutua kwenye mwezi na kiliamriwa kujiangamiza chenyewe badala yake.

Opereta hiyo ya kibinafsi, Astrobotic yenye makao yake Pittsburgh, ilikielekeza chombo hicho kwenye angahewa ya Dunia ili kuteketea.

Kituo cha ufuatiliaji huko Canberra, Australia, kilithibitisha kupotea kwa rada ya Peregrine saa 20:59 GMT.

Lengo la wanaanga lilikuwa kuwasilisha vifaa vitano kwa Nasa kwenye uso wa Mwezi, ili kuchunguza mazingira ya ndani kabla ya kurudi kwa wanaanga baadaye muongo huu.

Iwapo chombo hicho cha Peregrine kingefanikiwa kutua, ingekuwa misheni ya kwanza ya Marekani katika nusu karne kufanya hivyo, na mradi wa kwanza kabisa wa kibinafsi kufikia mafanikio hayo.


Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)