Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Jaribio la Marekani kurejea mwezini katika miaka 50 lagonga mwamba

 




Chombo cha anga za juu cha Marekani kilichozinduliwa wiki iliyopita kujaribu kutua Mwezini kimesitisha ujumbe wake baada ya kulipuka juu ya Bahari ya Pasifiki.

Chombo hicho kwa jina Peregrine One kilipata hitilafu ambayo iliharibu matarajio yoyote ya kutua kwenye mwezi na kiliamriwa kujiangamiza chenyewe badala yake.

Opereta hiyo ya kibinafsi, Astrobotic yenye makao yake Pittsburgh, ilikielekeza chombo hicho kwenye angahewa ya Dunia ili kuteketea.

Kituo cha ufuatiliaji huko Canberra, Australia, kilithibitisha kupotea kwa rada ya Peregrine saa 20:59 GMT.

Lengo la wanaanga lilikuwa kuwasilisha vifaa vitano kwa Nasa kwenye uso wa Mwezi, ili kuchunguza mazingira ya ndani kabla ya kurudi kwa wanaanga baadaye muongo huu.

Iwapo chombo hicho cha Peregrine kingefanikiwa kutua, ingekuwa misheni ya kwanza ya Marekani katika nusu karne kufanya hivyo, na mradi wa kwanza kabisa wa kibinafsi kufikia mafanikio hayo.


Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)