Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Mwanamke wa Marekani ahukumiwa miaka 26 kwa mauaji ya mama yake

 

Mwanamke mmoja nchini Marekani ambaye alisaidia kumuua mama yake na kuuweka mwili wake kwenye sanduku wakati wa likizo ya 2014 huko Bali amehukumiwa kifungo cha miaka 26 jela.

Heather Mack alipatikana na hatia nchini Indonesia mwaka 2015 na kuhukumiwa miaka 10 jela, lakini akaachiliwa huru mwaka wa 2021.

Kisha alikamatwa alipofika Marekani na kushtakiwa kwa njama ya kumuua raia wa Marekani.

Mack amekaa miaka miwili iliyopita katika gereza la Chicago alipokuwa akisubiri hukumu.

Siku ya Jumatano, Jaji Matthew Kennelly aliamua kwamba Mack, 28, atapokea afueni kwa muda ambao amehudumu hadi sasa, na hivyo kupunguza kifungo chake rasmi hadi takriban miaka 23.

Waendesha mashtaka walikuwa wamependekeza kifungo cha miaka 28 jela kwa Mack, ambaye alipanga njama na mpenzi wake wa wakati huo Tommy Schaefer kumuua mamake, msomi tajiri Sheila von Wiese-Mack.

Wawili hao inasemekana walifanya hivyo ili kupata $1.5m (£1.17m) mali iliyowekwa katika hazina ambayo bintiye angeipata baadaye.

Waendesha mashtaka walidai kuwa Bi Mack - ambaye alikuwa na umri wa miaka 18 wakati wa mauaji hayo na mjamzito - aliziba mdomo wa mamake huku Bw Schaefer akimpiga kichwani kwa bakuli la matunda.Mwili huo baadaye uligunduliwa ukiwa umeingizwa ndani ya sanduku.

Baada ya mauaji ya Wiese-Mack katika hoteli hiyo, Bi Mack na Bw Schaefer waliacha sanduku la mabaki yake kwenye buti ya teksi, waendesha mashtaka walisema.Baadaye dereva alitoa taarifa kwa polisi.

Wanandoa hao waligunduliwa baadaye wakiwa katika hoteli nyingine huko Bali.

Wakati wa hukumu yake, kakake Wiese-Mack, Bill Wiese, aliiomba mahakama kutoa adhabu ya juu iwezekanavyo, akisema kuwa Mack hajaonyesha kujutia uhalifu huo

Soma zaidi

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)