Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

TANZANIA YASITSHA SAFARI ZA NDEGE ZA SHIRKA LA NDEGE LA KENYA AIRWAYS KATIKA MZOZO MPYA




 Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Tanzania imetangaza kusitisha safari za ndege za abiria za Shirika la Ndege la Kenya (KQ) kuanzia Januari 22, mwaka huu.

Hatua hiyo inakuja baada ya Mamlaka ya Ndege nchini Kenya kukataa ombi la Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuruhusu ndege ya mizigo ya Air Tanzania kusafirisha mizigo kutoka Nairobi kwenda mataifa mengine.

Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Hamza Johari ameiambia BBC kuwa, uamuzi wa Tanzania unatokana na vikwazo vinavyowekwa na mamlaka za Kenya kuzuia shughuli za ndege ya abiria ya Air Tanzania.

Johari alisema, “Sababu za kuzuia ndege zao ni za msingi, KQ inakuja kwetu (Tanzania) bila vikwazo, lakini sisi ndege yetu ya Air Tanzania inawekewa vikwazo kinyume na Makubaliano yetu ya kibiashara ya huduma za ndege tuliyosaini Novemba mwaka 2016.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa wamekuwa wakitafuta mamlaka hiyo ya Kenya kwa ajili ya usuluhishi bila mafanikio.

“Tumewaandikia barua hawajibu, pia tumekutana nao bila mafanikio. Lakini kama wakitaka tubadili uamuzi wetu, basi waje mezani tukubaliane juu ya vikwazo vilivyopo kwani mpaka sasa tumepata hasara. Mfano kwa safari moja ya ndege ya mizigo tunapata hasara ya dola za kimarekani 330,000,” alisema Johari.

Mwaka 2020, mamlaka za Tanzania zilisimamisha safari za KQ kati ya Nairobi na viwanja vya Tanzania kama Dar es Salaam, Kilimanjaro na Zanzibar kwa kile ilichodai kuwa Kenya iliiwekea vikwazo mbalimbali vya kibiashara.

SHARE KWA WENGINE

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)