Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

TANZANIA YASITSHA SAFARI ZA NDEGE ZA SHIRKA LA NDEGE LA KENYA AIRWAYS KATIKA MZOZO MPYA




 Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Tanzania imetangaza kusitisha safari za ndege za abiria za Shirika la Ndege la Kenya (KQ) kuanzia Januari 22, mwaka huu.

Hatua hiyo inakuja baada ya Mamlaka ya Ndege nchini Kenya kukataa ombi la Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuruhusu ndege ya mizigo ya Air Tanzania kusafirisha mizigo kutoka Nairobi kwenda mataifa mengine.

Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Hamza Johari ameiambia BBC kuwa, uamuzi wa Tanzania unatokana na vikwazo vinavyowekwa na mamlaka za Kenya kuzuia shughuli za ndege ya abiria ya Air Tanzania.

Johari alisema, “Sababu za kuzuia ndege zao ni za msingi, KQ inakuja kwetu (Tanzania) bila vikwazo, lakini sisi ndege yetu ya Air Tanzania inawekewa vikwazo kinyume na Makubaliano yetu ya kibiashara ya huduma za ndege tuliyosaini Novemba mwaka 2016.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa wamekuwa wakitafuta mamlaka hiyo ya Kenya kwa ajili ya usuluhishi bila mafanikio.

“Tumewaandikia barua hawajibu, pia tumekutana nao bila mafanikio. Lakini kama wakitaka tubadili uamuzi wetu, basi waje mezani tukubaliane juu ya vikwazo vilivyopo kwani mpaka sasa tumepata hasara. Mfano kwa safari moja ya ndege ya mizigo tunapata hasara ya dola za kimarekani 330,000,” alisema Johari.

Mwaka 2020, mamlaka za Tanzania zilisimamisha safari za KQ kati ya Nairobi na viwanja vya Tanzania kama Dar es Salaam, Kilimanjaro na Zanzibar kwa kile ilichodai kuwa Kenya iliiwekea vikwazo mbalimbali vya kibiashara.

SHARE KWA WENGINE

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)