Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Israel yasitisha mapigano mjini Rafah huku wakaazi wakielezea mashambulizi 'yasiyofikirika''

 


Mjini Gaza Jeshi la Ulinzi la Israeli (IDF) limetangaza ‘’kusimamishwa kwa shughuli za kijeshi kwa muda’’kwa madhumuni ya kibinadamu" mjini Rafah hadi nane za mchana kwa saa za eneo.

Hatua hii inafuatia usiku wa mashambulizi ya Israeli katika mji wa kusini, ambapo watu wengi kutoka mahali maeneo mbali mbali ya Gaza wamekimbilia.

Samir Qeshta anasema nyumba yake "iliharibiwa kabisa" katika shambulio hilo.

"Nyumba hii ilinihifadhi mimi na watoto wangu. Nilikuwa nikijiandaa kwa ajili ya mwanangu wa kiume kuoa ndani yake, nilikuwa nimeipaka rangi," aliambia shirika la habari la AFP.

"Sisi ni watu wa amani, walitupiga bila tahadhari. Nilikuwa nikimtembelea dada yangu na mke wangu alikuwa nyumbani kwa wazazi wake."

Nimma al-Akhras alikuwa nyumbani wakati mashambulizi ya mabomu yalipoanza.

"Mashambulizi yalikuwa sio ya kufikirika," anasema. “Tulianza kupiga kelele na sikuweza kusogea hadi mtu akanibeba na kuniweka kwenye mkokoteni.

"Tumekosea nini? Tulikuwa tumekaa tu. Si salama majumbani mwetu wala nje, sijui twende wapi?"

Israel inasema inawalenga magaidi na miundombinu yao - na kwamba inajaribu kupunguza vifo vya raia.

Soma zaidi

SHARE kwa wengine

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)