Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Israel yasitisha mapigano mjini Rafah huku wakaazi wakielezea mashambulizi 'yasiyofikirika''

 


Mjini Gaza Jeshi la Ulinzi la Israeli (IDF) limetangaza ‘’kusimamishwa kwa shughuli za kijeshi kwa muda’’kwa madhumuni ya kibinadamu" mjini Rafah hadi nane za mchana kwa saa za eneo.

Hatua hii inafuatia usiku wa mashambulizi ya Israeli katika mji wa kusini, ambapo watu wengi kutoka mahali maeneo mbali mbali ya Gaza wamekimbilia.

Samir Qeshta anasema nyumba yake "iliharibiwa kabisa" katika shambulio hilo.

"Nyumba hii ilinihifadhi mimi na watoto wangu. Nilikuwa nikijiandaa kwa ajili ya mwanangu wa kiume kuoa ndani yake, nilikuwa nimeipaka rangi," aliambia shirika la habari la AFP.

"Sisi ni watu wa amani, walitupiga bila tahadhari. Nilikuwa nikimtembelea dada yangu na mke wangu alikuwa nyumbani kwa wazazi wake."

Nimma al-Akhras alikuwa nyumbani wakati mashambulizi ya mabomu yalipoanza.

"Mashambulizi yalikuwa sio ya kufikirika," anasema. “Tulianza kupiga kelele na sikuweza kusogea hadi mtu akanibeba na kuniweka kwenye mkokoteni.

"Tumekosea nini? Tulikuwa tumekaa tu. Si salama majumbani mwetu wala nje, sijui twende wapi?"

Israel inasema inawalenga magaidi na miundombinu yao - na kwamba inajaribu kupunguza vifo vya raia.

Soma zaidi

SHARE kwa wengine

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)