Posts

Showing posts from January, 2024

Mpalestina aliyeshinda tuzo ya Grammy ashambuliwa na walowezi wa Israel na kukamatwa na jeshi

Image
 Mshindi wa tuzo ya Oscar ya Palestina ameshambuliwa na walowezi wa Israel, wanaharakati walioshuhudia tukio hilo wanasema, kabla ya kukamatwa na jeshi la Israel. Hamdan Ballal, mmoja wa wakurugenzi wenza wanne wa shirika la ‘No Other Land{hakuna Ardhi Nyingine} , alikuwa na nyumba yake katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel ikiwa imezingirwa na walowezi wakati wa shambulio la Jumatatu, Kituo cha Kundi la Waasi wa Kiyahudi (CJNV) kilisema. Mkurugenzi mwenza Yuval Abraham alisema Bw Ballal alipigwa na walowezi kisha kuchukuliwa na wanajeshi akiwa kwenye gari la wagonjwa. Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lilisema hakuna Mpalestina aliyezuiliwa kutoka kwa gari la wagonjwa. Bila kumtaja Bw Ballal, IDF ilisema Wapalestina watatu na Muisraeli wamezuiliwa kwa tuhuma za "kurusha mawe" kwa vikosi vya usalama. Mwanaharakati ambaye alikuwa katika eneo la tukio aliambia BBC kuwa Wapalestina watatu waliozuiliwa, akiwemo Bw Ballal, walijeruhiwa katika shambulio la walowezi na sasa ...

UNRWA ni nini na kwa nini ufadhili wake umesimamishwa?

Image
  CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Maelezo ya picha, Umoja wa Mataifa hutoa huduma muhimu Gaza kama vile maji wakati miundombinu ikiwa karibu kushindwa kufany akazi baada ya zaidi ya siku 100 za mashambulizi ya anga ya Israel Saa 8 zilizopita Na Aine Gallagher BBC Global Digital Wakati nchi za Magharibi zikisitisha ufadhili kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina, baada ya madai ya Israel kwamba wafanyakazi wake wachache walishiriki katika shambulio la Hamas dhidi ya Israel mnamo Oktoba 7, tunaangalia kile UNRWA inafanya na jinsi inavyofadhiliwa. UNRWA ni nini? UNRWA inasimama kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usaidizi na Kazi kwa Wakimbizi wa Palestina katika eneo la karibu la Mashariki . Inaendesha shule, huduma za kijamii, vituo vya afya na kusambaza misaada ya chakula kwa wakimbizi wa Palestina milioni 5.9 mjini Gaza, Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel, pamoja na Lebanon, Syria na Jordan. Ilianzishwa wakati gani? Ilianzishwa mwaka 1949 kwa aji...

Wasiwasi waibuka huku M23 ikiunda utawala mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Image
  Kundi la waasi la M23 limeteua utawala wake katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wake mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na hivyo kuzua wasiwasi Katika taarifa ya kundi hilo, kiongozi wa kisiasa wa M23 Bertrand Bisimwa amesema kundi hilo limeteua watawala katika eneo la Rutshuru la Kivu Kaskazini. Aliongeza kuwa viongozi wa miji ya Kiwanja, Rubare na Bunagana, katika Kivu Kaskazini, wameteuliwa pia. Waasi wanadhibiti sehemu kubwa ya Rutshuru na Masisi, mbili kati ya wilaya tano zinazounda jimbo la Kivu Kaskazini, na ziko takriban kilomita 35 (maili 22) magharibi mwa mji mkuu wa mkoa huo, Goma. Katika siku za hivi karibuni, jeshi la Congo limeanzisha mashambulizi makubwa ya ndege zisizo na rubani katika maeneo yanayodhibitiwa na M23. Siku ya Jumatano msemaji wa kundi hilo alisema wapiganaji wake waliiangusha moja ya ndege zisizo na rubani tatu zilizokuwa zikitumiwa na jeshi. BBC haijathibitisha dai hili kwa duru huru, wala jeshi halijatoa maoni kulihusu. Mitandao ya...

Mnada wa vitu vya Mandela: Afrika Kusini yataka kuzuia uuzaji juu ya urithi

Image
  Serikali ya Afrika Kusini inajaribu kusitisha mnada wenye utata wa vitu 70 vya kibinafsi vya shujaa wa kupinga ubaguzi wa rangi Nelson Mandela. Ni pamoja na seti ya vifaa vya usikivu, kitambulisho, zawadi kutoka kwa viongozi wa dunia na baadhi ya mavazi ya rais wa kwanza wa kidemokrasia, kama vile mashati yake ya "Madiba". Binti yake mkubwa, Makaziwe Mandela, anapiga mnada bidhaa hizo nchini Marekani. Lakini serikali ya Afrika Kusini inasema bidhaa hizo ni mali ya taifa hilo. Chini ya sheria ya nchi, vitu vinavyochukuliwa kuwa vya urithi wa kitaifa haviwezi kuchukuliwa nje ya Afrika Kusini. Wakala wa Rasilimali za Urithi wa Afrika Kusini (Sahra), chombo cha serikali kilichopewa dhamana ya kulinda historia na utamaduni wa nchi hiyo, kilisema kuwa kimewasilisha rufaa ya kuzuia uuzaji huo. Ombi hilo limeungwa mkono na wizara ya michezo, sanaa na utamaduni. Waziri Zizi Kodwa alisema anaunga mkono kesi hiyo "kwa ajili ya kudumisha urithi tajiri wa nchi". Aliongeza kuwa...

Je, ni kweli kuwa Hamas iliundwa na Israel?

Image
  Madai kwamba vuguvugu la Hamas ulikuwa mradi wa Israel yamekuwa yakisambazwa kwenye vyombo vya habari na wasomi - tangu wapiganaji hao wawaue na kuwateka nyara Waisraeli tarehe 7 Oktoba. Kuna ukweli gani nyuma ya madai hayo? Wanachama wengi wa Hamas wanakataa madai hayo kama wanavyokataa maafisa wa ngazi za juu wa Israel. Lakini madai hayo yaliwahi kusemwa hadharani na Rais wa zamani wa Misri, Hosni Mubarak. Pia, Seneta wa chama cha Republican katika Bunge la Marekani alipata kutoa madai hayo na vilevile yamejadiliwa na maafisa wa usalama wa ndani wa Israel, Shin Bet. Pia Unaweza Kusoma Uharibifu wa maeneo ya kidini huko Gaza 17 Januari 2024 Walikuwa macho ya Israeli kwenye mpaka - lakini tahadhari zao kuhusu Hamas hazikusikika 15 Januari 2024 Maafisa wa Israel wanataka kuiangamiza Gaza- Mahakama ya ICJ yafahamishwa 11 Januari 2024 Udugu wa Kiislamu Mapambano ya muda mrefu ya Hamas yana mizizi yake katikati ya miaka ya 1940 katika maeneo ya Wapalestina, wakati matawi ya kwanza ya...