Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Wanajeshi watatu wa Marekani wauawa katika shambulio la ndege zisizo na rubani Mashariki ya Kati




Wanajeshi watatu wa Marekani wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika shambulio la ndege isiyo na rubani kwenye kituo cha Marekani karibu na mpaka wa Jordan na Syria.

Rais wa Marekani Joe Biden alisema shambulio hilo lilitekelezwa na "makundi ya wapiganaji wenye itikadi kali wanaoungwa mkono na Iran". Aliongeza: "Tutajibu."

Ni mara ya kwanza kwa shambulio kuua wanajeshi wa Marekani katika eneo hilo tangu shambulio la Hamas la tarehe 7 Oktoba dhidi ya Israel.

Jordan inasema shambulio hilo lilifanyika Syria, sio ndani ya Jordan.

Kumekuwa na mashambulizi mengine kwenye kambi za Marekani katika eneo hilo lakini hadi sasa hakuna majeraha walioripotiwa na jeshi la Marekani.

Haijabainika ni nani aliyetekeleza shambulio hili la hivi punde.

Rais Biden alisema Marekani "itawawajibisha wale wote wanaohusika kwa wakati na kwa njia tunayochagua".
S0MA ZAIDI HAPA

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)