Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

Marekani yaidhinisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa Iran nchini Syria na Iraq


.
Image caption: Wanajeshi wa Marekani

Marekani imeidhinisha mipango ya mfululizo wa mashambulizi dhidi ya malengo ya Iran nchini Syria na Iraq, maafisa wameiambia mshirika wa BBC Marekani CBS News.

Mashambuliizi hayo yatafanyika kwa siku kadhaa, maafisa wanasema, na hali ya hewa huenda itaamuru ini lini yatazinduliwa.

Hatua hiyo inajiri baada ya shambulio la ndege isiyo na rubani kuwaua wanajeshi watatu wa Marekani huko Jordan, karibu na mpaka wa Syria, siku ya Jumapili.Marekani imelilaumu kundi la wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran kwa shambulio hilo.

Kundi la Islamic Resistance in Iraq - ambalo linaaminika kuwa na wanamgambo wengi ambao wamejihami, kufadhiliwa na kupewa mafunzo na kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Iran - limesema ndilo lililohusika na shambulio hilo.

Iran imekanusha kuhusika na shambulio hilo lililojeruhi wanajeshi wengine 41 wa Marekani katika kambi ya kijeshi.

Wakati maafisa wa Marekani wameahidi kujibu mashambulizi hayo ya ndege zisizo na rubani, Rais Joe Biden na maafisa wengine wamesema kuwa nchi hiyo haitafuti vita zaidi na Iran.

Makundi kadhaa yanayoungwa mkono na Iran yameongeza mashambulizi dhidi ya mashirika yenye uhusiano na Marekani na Israel tangu kuanza kwa vita vya Israel na Hamas tarehe 7 Oktoba.

Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran nchini Yemen, kwa mfano, wameshambulia meli katika Bahari ya shamu na Ghuba ya Aden, na kusababisha mashambulizi kutoka kwa Marekani na washirika wake.

Afisa wa ulinzi wa Marekani aliiambia CBS kwamba ndege isiyo na rubani ilidunguliwa usiku kucha katika Ghuba ya Aden, huku ndege isiyo na rubani ya baharini ikipigwa na kuharibiwa katika Bahari ya shamu.

Miili ya wanajeshi watatu wa Marekani waliouawa katika shambulizi hilo inatarajiwa kurejeshwa katika kambi ya Jeshi la Wanahewa la Delaware siku ya Ijumaa. Ikulu ya White House imetangaza kuwa Rais Biden atahudhuria.

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)