Mpalestina aliyeshinda tuzo ya Grammy ashambuliwa na walowezi wa Israel na kukamatwa na jeshi

Image
 Mshindi wa tuzo ya Oscar ya Palestina ameshambuliwa na walowezi wa Israel, wanaharakati walioshuhudia tukio hilo wanasema, kabla ya kukamatwa na jeshi la Israel. Hamdan Ballal, mmoja wa wakurugenzi wenza wanne wa shirika la ‘No Other Land{hakuna Ardhi Nyingine} , alikuwa na nyumba yake katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel ikiwa imezingirwa na walowezi wakati wa shambulio la Jumatatu, Kituo cha Kundi la Waasi wa Kiyahudi (CJNV) kilisema. Mkurugenzi mwenza Yuval Abraham alisema Bw Ballal alipigwa na walowezi kisha kuchukuliwa na wanajeshi akiwa kwenye gari la wagonjwa. Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lilisema hakuna Mpalestina aliyezuiliwa kutoka kwa gari la wagonjwa. Bila kumtaja Bw Ballal, IDF ilisema Wapalestina watatu na Muisraeli wamezuiliwa kwa tuhuma za "kurusha mawe" kwa vikosi vya usalama. Mwanaharakati ambaye alikuwa katika eneo la tukio aliambia BBC kuwa Wapalestina watatu waliozuiliwa, akiwemo Bw Ballal, walijeruhiwa katika shambulio la walowezi na sasa ...

Tshisekedi na Kagame wakutana na kukubaliana kusitisha vita DRC


 Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame walikutana nchini Qatar Jumanne hii kwa mazungumzo yao ya kwanza ya ana kwa ana tangu waasi wa M23 waanze mashambulizi mashariki mwa Kongo mwezi Januari, taarifa ya pamoja ya serikali tatu ilisema.

Mkutano huo uliosimamiwa na Amir wa Qatar, unakuja siku moja baada ya kundi la M23 kujitoa kwenye mazungumzo mengine ya Angola, ikiwa tayari imeteka miji miwili mikubwa mashariki mwa Kongo.

Kongo inaishutumu Rwanda kwa kutuma silaha na wanajeshi wa Rwanda kuwaunga mkono waasi hao, ambao mashambulizi yao yameitumbukiza mashariki mwa Kongo katika mzozo wake mbaya zaidi katika miongo kadhaa.

Rwanda imesema kuwa vikosi vyake vinafanya kazi ya kujilinda dhidi ya jeshi la Kongo na wanamgambo wanaoishambulia Kigali., ikikana kuiunga mkono M23.

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)