Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Tshisekedi na Kagame wakutana na kukubaliana kusitisha vita DRC


 Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame walikutana nchini Qatar Jumanne hii kwa mazungumzo yao ya kwanza ya ana kwa ana tangu waasi wa M23 waanze mashambulizi mashariki mwa Kongo mwezi Januari, taarifa ya pamoja ya serikali tatu ilisema.

Mkutano huo uliosimamiwa na Amir wa Qatar, unakuja siku moja baada ya kundi la M23 kujitoa kwenye mazungumzo mengine ya Angola, ikiwa tayari imeteka miji miwili mikubwa mashariki mwa Kongo.

Kongo inaishutumu Rwanda kwa kutuma silaha na wanajeshi wa Rwanda kuwaunga mkono waasi hao, ambao mashambulizi yao yameitumbukiza mashariki mwa Kongo katika mzozo wake mbaya zaidi katika miongo kadhaa.

Rwanda imesema kuwa vikosi vyake vinafanya kazi ya kujilinda dhidi ya jeshi la Kongo na wanamgambo wanaoishambulia Kigali., ikikana kuiunga mkono M23.

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

INSIGNIA LIMITED COMPANY

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)