Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Mpalestina aliyeshinda tuzo ya Grammy ashambuliwa na walowezi wa Israel na kukamatwa na jeshi


 Mshindi wa tuzo ya Oscar ya Palestina ameshambuliwa na walowezi wa Israel, wanaharakati walioshuhudia tukio hilo wanasema, kabla ya kukamatwa na jeshi la Israel.


Hamdan Ballal, mmoja wa wakurugenzi wenza wanne wa shirika la ‘No Other Land{hakuna Ardhi Nyingine} , alikuwa na nyumba yake katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel ikiwa imezingirwa na walowezi wakati wa shambulio la Jumatatu, Kituo cha Kundi la Waasi wa Kiyahudi (CJNV) kilisema.


Mkurugenzi mwenza Yuval Abraham alisema Bw Ballal alipigwa na walowezi kisha kuchukuliwa na wanajeshi akiwa kwenye gari la wagonjwa.


Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lilisema hakuna Mpalestina aliyezuiliwa kutoka kwa gari la wagonjwa. Bila kumtaja Bw Ballal, IDF ilisema Wapalestina watatu na Muisraeli wamezuiliwa kwa tuhuma za "kurusha mawe" kwa vikosi vya usalama.


Mwanaharakati ambaye alikuwa katika eneo la tukio aliambia BBC kuwa Wapalestina watatu waliozuiliwa, akiwemo Bw Ballal, walijeruhiwa katika shambulio la walowezi na sasa wako katika kituo cha polisi cha Israel katika Ukingo wa Magharibi.


Wanashukiwa kurusha mawe na kumjeruhi mchungaji mdogo wa walowezi na wanahojiwa, mwanaharakati huyo alisema, akiongeza kuwa wamepata wakili.


Shambulio hilo lilianza mwendo wa saa 18:00 (16:00 GMT) siku ya Jumatatu, wakati walowezi karibu dazeni waliojifunika nyuso zao walipoanzisha mashambulizi katika kijiji cha Susya, wanaharakati watano wa Kiyahudi kutoka Marekani kutoka CJNV walisema.


Watano hao walisema walienda kijijini hapo kuelezea kuhusu tukio hilo kabla ya, huku walowezi wakivunja vioo vya magari yao na kuwapiga ngumi na fimbo.


Nyumba ya Bw Ballal inaripotiwa kuzungukwa na walowezi. Yuval Abraham, mkurugenzi wa Israel ambaye alishinda tuzo ya Oscar mwezi huu pamoja na Bw Ballal, alisema watu kadhaa wamejeruhiwa na mali kuharibiwa katika shambulio hilo.

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

INSIGNIA LIMITED COMPANY

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)