Trump apotosha kwa kutumia picha ya Congo na kudai ni ya mauaji ya kimbari ya Wazungu wa Afrika Kusini

Image
  Rais wa Marekani Donald Trump alionyesha picha iliyochukuliwa katika video ya shirika la habari la Reuters katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na kuiwasilisha kama ushahidi wa mauaji ya halaiki ya Wazungu wa Afrika Kusini. "Hawa wote ni wakulima wa kizungu ambao wanazikwa," Trump alisema siku ya Jumatano, akionesha picha hiyo wakati wa mkutano katika Ikulu ya Marekani na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa. Picha hiyo ilitokana na video iliyochapishwa na Reuters Februari 3, 2025, inaonyesha wafanyakazi wa kibinadamu wakinyanyua mifuko yenye miili katika mji wa Goma nchini Congo. Picha hiyo ilitolewa kutoka katika video ya Reuters iliyopigwa kufuatia mapigano makali na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda. Picha hiyo iliyooneshwa na Trump lilichapishwa na American Thinker, jarida la kihafidhina la mtandaoni – likionesha migogoro na mivutano ya kirangi Afrika Kusini na Congo. Ikulu ya White House haikujibu maswali ya Reuters kuhusu picha hiyo. Andrea Widburg, mhariri ...

Trump atangaza ushuru zaidi kwa alumini na chuma kutoka Canada

 Rais wa Marekani Donald Trump amesema atazidisha ushuru kwenye chuma na alumini bidhaa zinazotoka Canada kutoka asilimia 25% hadi asilimia 50%.

Katika vita vya kibiashara vinavyoendelea, Trump amesema hatua hii ni kulipiza kisasi kwa ushuru wa asilimia 25 ambao Ontario iliweka kwa umeme inayoupeleka kwa majimbo ya kaskazini ya Marekani.

Akijibu tangazo la Trump, waziri mkuu wa Ontario amesema “hatutajinyenyekea” na kumtaka Trump “aache fitina”.

Trump amesema ushuru huu utaanza Jumatano, na kuongeza kwamba atatangaza hali ya “dharura ya kitaifa kuhusu umeme” katika majimbo hayo.

Hatua hii inajiri baada ya siku mbaya zaidi ya mwaka 2025 kwa masoko ya Marekani, yaliyosababishwa na hofu ya ushuru mkali wa Rais Donald Trump dhidi ya washirika wake wakubwa wa kibiashara.

Alipohojiwa kuhusu uwezekano wa kudorora kwa uchumi wa Marekani, Trump alisema uchumi uko katika “kipindi cha mabadiliko.”


source

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)