Tundu Lissu afikishwa Mahakamani asomewa shitaka la uhaini

Image
  Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini tanzania, Chadema, Tundu Lissu jioni hii amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, na kusomewa shitaka moja la uhaini. Tundu anayetetewa kwa sasa na Mawakili sita ambao ni Dk. Rugemeleza Nshalla, Dickson Matata, Jebra Kambole, Michael Lugina, Hekima Mwasipu, na Gaston Garubindi, alisomewa shitaka hilo la Wakili Nassoro Katuga Awali Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilisema lilimkamata Lissu jana mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025. Aidha Polisi nchini humo kupitia taarifa yake ilitoa onyo kwa vyama vyote vya siasa kutotoa maneno ya uchochezi, kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. Mapema Polisi walipiga mabomu ya machozi na kuwatawanya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema huku wakizua viongozi wa chama hicho kufanya mkutano na waandishi wa habari. Vyombo vy...

TikTok yasitisha huduma zake Marekani saa chache kabla ya kupigwa marufuku

 

TikTok haipatikani mtandaoni nchini Marekani, saa chache kabla ya sheria mpya ya kupiga marufuku jukwaa hilo kuanza kutumika.

Ujumbe ulioonekana kwenye programu kwa watumiaji wa Marekani ulisema sheria ya kupiga marufuku TikTok imepitishwa, kumaanisha "huwezi kutumia TikTok kwa sasa".

"Tuna bahati kwamba Rais Trump amedokeza kuwa atashirikiana nasi kutafuta suluhisho la kurejesha TikTok mara tu atakapoingia madarakani," ilisomeka.

Hili linawadia baada ya mtandao huo wa kijamii kuonya kwamba huduma zake "zitapotea" siku ya Jumapili isipokuwa kama utawala unaoondoka wa Biden utatoa hakikisho kwamba marufuku hiyo haitatekelezwa.

Rais mteule Donald Trump amesema "uwezekano mkubwa zaidi" ni kwamba ataipa TikTok siku 90 ili kuepuka marufuku hiyo mara tu atakapoingia madarakani Jumatatu.

Watumiaji waliripoti kuwa programu hiyo pia ilikuwa imeondolewa kwenye Apple na Google ya Marekani huku TikTok.com haikuwa inaonyesha video.

"Kuongeza muda wa siku 90 ni jambo ambalo kuna uwezekano mkubwa litatekelezwa, kwa sababu ndio hatua sahihi kuchukuliwa," Trump aliambia NBC News siku ya Jumamosi.

"Nikiamua kufanya hivyo, kuna uwezekano nikatangaza Jumatatu."

Ikulu ya White House ilisema ni jukumu la utawala unaokuja kuchukua hatua.

"Hatuoni sababu ya TikTok au kampuni zingine kuchukua hatua katika siku chache zijazo kabla ya utawala wa Trump kuchukua madaraka Jumatatu," katibu wa waandishi wa habari Karine Jean-Pierre alisema katika taarifa.

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

INSIGNIA LIMITED COMPANY

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)