Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

TikTok yasitisha huduma zake Marekani saa chache kabla ya kupigwa marufuku

 

TikTok haipatikani mtandaoni nchini Marekani, saa chache kabla ya sheria mpya ya kupiga marufuku jukwaa hilo kuanza kutumika.

Ujumbe ulioonekana kwenye programu kwa watumiaji wa Marekani ulisema sheria ya kupiga marufuku TikTok imepitishwa, kumaanisha "huwezi kutumia TikTok kwa sasa".

"Tuna bahati kwamba Rais Trump amedokeza kuwa atashirikiana nasi kutafuta suluhisho la kurejesha TikTok mara tu atakapoingia madarakani," ilisomeka.

Hili linawadia baada ya mtandao huo wa kijamii kuonya kwamba huduma zake "zitapotea" siku ya Jumapili isipokuwa kama utawala unaoondoka wa Biden utatoa hakikisho kwamba marufuku hiyo haitatekelezwa.

Rais mteule Donald Trump amesema "uwezekano mkubwa zaidi" ni kwamba ataipa TikTok siku 90 ili kuepuka marufuku hiyo mara tu atakapoingia madarakani Jumatatu.

Watumiaji waliripoti kuwa programu hiyo pia ilikuwa imeondolewa kwenye Apple na Google ya Marekani huku TikTok.com haikuwa inaonyesha video.

"Kuongeza muda wa siku 90 ni jambo ambalo kuna uwezekano mkubwa litatekelezwa, kwa sababu ndio hatua sahihi kuchukuliwa," Trump aliambia NBC News siku ya Jumamosi.

"Nikiamua kufanya hivyo, kuna uwezekano nikatangaza Jumatatu."

Ikulu ya White House ilisema ni jukumu la utawala unaokuja kuchukua hatua.

"Hatuoni sababu ya TikTok au kampuni zingine kuchukua hatua katika siku chache zijazo kabla ya utawala wa Trump kuchukua madaraka Jumatatu," katibu wa waandishi wa habari Karine Jean-Pierre alisema katika taarifa.

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

INSIGNIA LIMITED COMPANY

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)