Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Israel yasema ushahidi unaonyesha mlipuko wa hospitali ulitoka Gaza huku Netanyahu akianza mazungumzo na Biden

 




Rais wa Marekani Joe Biden amemwambia waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwamba "inaonekana" "shambulio la hospitali ya Al Ahli lilitekelezwa na kundi jingine ".

Biden anasema "amehuzunishwa sana na kukasirishwa" na tukio hilo.

"Kulingana na kile nimeona inaonekana kana kwamba shambulio hilo lilitekelezwa na kundi jingi, sio wewe. Lakini kuna watu wengi huko nje ambao hawana uhakika, kwa hivyo lazima tukabiliane na mambo mengi," alisema.

BBC inajaribu kuunganisha vipande vidogo vidogo vya mlipuko wa hospitali ya jana usiku - ambao Hamas na mamlaka ya Palestina wanailaumu Israel kwa kutekeleza shambulio la angani.

Rais Biden anasema alitembelea Israel ili kuonyesha mahali Marekani iinaunga mkono katika mzozo huo.

Anaendelea kuelezea mauaji ya Hamas tarehe 7 Oktoba. Anasema "siyo sifa " kusema "walichinja" watu 1,300, ikiwa ni pamoja na Wamarekani 31.

Pia alizungumzia kuhusu mateka wa Israeli, pamoja na watoto.

"Hebu fikiria watoto hao waliokuwa wanajificha kutoka kwa Hamas walikuwa wanafikiria nini? Ni zaidi ya ufahamu wangu.

"Marekani itaendelea kuiunga mkono Israel, anasema, akimwambia Netanyahu: "Ninatazamia kuwa na mjadala kuhusu kile kinachotokea hapa.

"Anasema "ujasiri, kujitolea na ushujaa" wa watu wa Israeli "ni wa kustaajabisha", akiongeza "Najivunia kuwa hapa".

Comments

UWABATA TV

UWABATA TANGAZO

INSIGNIA LIMITED COMPANY

Kwanini ulaji wa nyama za watu katika nchi za Ulaya ulitumika kama tiba ya hali ya juu?

GRUMETI FUND TRUST,

Total Tanzania Careers 2021, Total Tanzania Jobs 2021

TECHNICIAN II (ELECTRICAL)