Posts

Showing posts from June, 2024

Trump apotosha kwa kutumia picha ya Congo na kudai ni ya mauaji ya kimbari ya Wazungu wa Afrika Kusini

Image
  Rais wa Marekani Donald Trump alionyesha picha iliyochukuliwa katika video ya shirika la habari la Reuters katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na kuiwasilisha kama ushahidi wa mauaji ya halaiki ya Wazungu wa Afrika Kusini. "Hawa wote ni wakulima wa kizungu ambao wanazikwa," Trump alisema siku ya Jumatano, akionesha picha hiyo wakati wa mkutano katika Ikulu ya Marekani na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa. Picha hiyo ilitokana na video iliyochapishwa na Reuters Februari 3, 2025, inaonyesha wafanyakazi wa kibinadamu wakinyanyua mifuko yenye miili katika mji wa Goma nchini Congo. Picha hiyo ilitolewa kutoka katika video ya Reuters iliyopigwa kufuatia mapigano makali na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda. Picha hiyo iliyooneshwa na Trump lilichapishwa na American Thinker, jarida la kihafidhina la mtandaoni – likionesha migogoro na mivutano ya kirangi Afrika Kusini na Congo. Ikulu ya White House haikujibu maswali ya Reuters kuhusu picha hiyo. Andrea Widburg, mhariri ...

Israel na Hezbollah wakaribia kupigana, wote wakataa kurudi nyuma

Image
  CHANZO CHA PICHA, AFP Maelezo ya picha, Wanajeshi wa Israel 23 Juni 2024 Vita kamili kati ya Israel na Hezbollah vitasababisha "janga", Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema. Lakini kwa David Kamari, ambaye anaishi chini ya moto unaokaribia kila siku upande wa mpaka wa Israel, vita hivyo vitakuwa suluhu. Mwezi uliopita, roketi ya Hezbollah iliyorushwa kutoka Lebanon ilitua kwenye bustani yake katika mji wa mpakani wa Kiryat Shmona, na kupasua nyumba yake katika maeneo kadhaa na kuijaza na vifusi. Anaonyesha mashimo ambayo vipande vya misumari vilipita kwenye kuta, vikimkosa kwa inchi chache. Na kisha kwenye vilima vilivyo juu yetu, ambapo eneo linalodhibitiwa na Hezbollah linaanzia. "Kila siku, kila usiku: mabomu. [Ni] tatizo," alisema. "Na mimi nilizaliwa hapa. Ikiwa unaishi hapa usiku mmoja, utakuwa na wazimu." David bado anaishi katika nyumba yake iliyojaa vifusi, vipande vya misumari vilivyonaswa na mabaki ya televisheni yake. Nje ni masalio meusi ...