Posts

Showing posts from May, 2025

Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

Trump apotosha kwa kutumia picha ya Congo na kudai ni ya mauaji ya kimbari ya Wazungu wa Afrika Kusini

Image
  Rais wa Marekani Donald Trump alionyesha picha iliyochukuliwa katika video ya shirika la habari la Reuters katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na kuiwasilisha kama ushahidi wa mauaji ya halaiki ya Wazungu wa Afrika Kusini. "Hawa wote ni wakulima wa kizungu ambao wanazikwa," Trump alisema siku ya Jumatano, akionesha picha hiyo wakati wa mkutano katika Ikulu ya Marekani na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa. Picha hiyo ilitokana na video iliyochapishwa na Reuters Februari 3, 2025, inaonyesha wafanyakazi wa kibinadamu wakinyanyua mifuko yenye miili katika mji wa Goma nchini Congo. Picha hiyo ilitolewa kutoka katika video ya Reuters iliyopigwa kufuatia mapigano makali na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda. Picha hiyo iliyooneshwa na Trump lilichapishwa na American Thinker, jarida la kihafidhina la mtandaoni – likionesha migogoro na mivutano ya kirangi Afrika Kusini na Congo. Ikulu ya White House haikujibu maswali ya Reuters kuhusu picha hiyo. Andrea Widburg, mhariri ...