Posts

Showing posts from May, 2022

Trump aitaka Iran kuingia makubaliano ya nyuklia, akionya kuhusu mashambulizi ya kikatili zaidi

  Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia, akisema aliipa Tehran nafasi baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu makubaliano yalikuwa yanakaribia kuingia awamu ya sita Jumapili. "Niliwaambia, kwa maneno makali, "fanyeni tu," ingawa walijaribu sana, haijalishi walikuwa karibu vipi, hawakuweza kufanikiwa," Trump anaandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth. "Iran lazima ifanye makubaliano na kuokoa kile ambacho hapo awali kilijulikana kama Dola ya Iran. Hakuna kifo tena, hakuna uharibifu tena, FANYA TU, KABLA HAMJACHELEWA." Hapo awali Trump alisema anafahamu mipango ya Israel kabla ya kuanza mashambulizi usiku kucha, lakini aliweka wazi kuwa wanajeshi wa Marekani hawakushiriki katika operesheni hiyo.

ORODHA YA MAJINA YA MAOMBI YA KAZI YA MUDA YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 YALIYOHAKIKIWA NA KUJIBIWA KIKAMILIFU

 ORODHA YA MAJINA YA MAOMBI YA KAZI YA MUDA YA SENSA  DOWNLOAD PDF FILE KUANGALIA JINA LAKO  HAPA CHINI CLICK ME

NAFASI YA KAZI YA MUDA KWENYE ZOEZI LA SENSA YA WATU NA MAKAZI TANZANIA

 UTANGULIZI Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iko kwenye maandalizi ya kufanya Sensa ya Watu na Makazi ambayo itafanyika tarehe 23 Agosti 2022. Ili kufanikisha Sensa hii, Serikali inatangaza nafasi za kazi za muda za MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA kwa Watanzania wenye nia na sifa zinazostahili kama ilivyoainishwa katika tangazo hili.  1. KARANI WA SENSA a) Kazi za Kufanya Mwombaji wa nafasi hii, endapo atachaguliwa atatakiwa kuhudhuria mafunzo ya makarani ambapo baada ya mafunzo ikiwa atafaulu atatakiwa kurejea katika eneo alilotokea au kupangiwa eneo lingine lolote kwa ajili ya kutekeleza kazi zifuatazo :- i) Kutambua mipaka ya eneo la kuhesabia watu kwa kulinganisha na ramani ya eneo la kuhesabia watu na maelezo ya mipaka yaliyopo kwenye ramani hiyo ; ii) Kushirikiana na msimamizi na uongozi wa eneo husika kutambua kama katika eneo la kuhesabia watu kuna makundi maalaum yanayotakiwa kuhesabiwa kwa utaratibu maalum tofauti na kaya za kawaida ; iii) Kuhoji dodoso l...